Mwandishi: Jotham Mwashighadi

Picha ni kwa hisani ya Youtube.com

 

Niko ziara ardhini, waridi kukutafutia

kalala huko nyikani, nikateswa na vidudu

nalialia jangwani, uso umesawajika

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Nimegaga upwani, kusaka mkate mweupe

Viganja vimatesoni, mtulinga umepindika

Kutumwa nimetumika, nikutunze ubavu

Elewa langu waridi, maua ni  nadra mno

 

Nilimilki bustani, ilosheheni uturi

Rangi za kububujika, mandhari ya paradiso

Nyuni na vikembe, walihani tenzi  za upendo

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Majira yana misimu, misimu ina vipindi

Naitamani shairi, tuitie chachu majini

Mboni tuangaliane, hapa tu tutafaraji

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Kibaba cha didimia, kwa miale ya msimu

Siha zetu tabaani, chumi na uwekezaji

Nibuni vipi wapenzi, msimu wa furaha?

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Nidhinishe  kipepeo, japo bustani limetota

Jipambe kwa hi na wanja, nami kwa tabasamu

Tuogelee hewani, tukuze chuki ya halaiki

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Wazistahili nyota, za mji wa mbinguni

Sasa udhuru naomba,nikupe ua lining’inialo kama popo

vumilivu kama mbavu, Korosho na tundale jekundu

Elewa langu waridi, maua ni nadra mno

 

Mbegu ni zao kamili, kanju ua la bakshishi

manjano au nyekundu, ishara ya hisia za joto

Korosho ina rotuba, hifadhiwa hadi kesho

Kanju ua la nyauka, hudonwa si kesho

Tukitua kipepeo, pokea korosho na uale

Author

A freelance writer, journalist, poet and blogger venturing mainly in social and community issues, study and analysis of behaviour and life, and the plight of the under-dogs in the society. 'I feed on human stories.'

Write A Comment