Tag

waliopendana


Browsing

Mwandishi:Sultan Karama Maji Male (kero)

 

1. Taanda kumswifu, Rabi mola Jalali
Thumma swalatu alifu, zimfikie rasuli
Na swahabaze ashirafu, kina Ali na Bilali
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?
2. Japo damu huchemka, tumeamua kutulia
Sio kuwa tunataka, kumuasi Jalia
Ila mambo kadhalika, mangi yanotufikia
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?
3. Mwaogopa ya duniani, ndilo la muhimu sana
Hebu pima fikirani, ndo mwamuudhi Rabana
Eti kisa tu chuoni, hatufai kuoana
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?
4. Tumechoka kuzini, vijana tumetubia
Tumerudi ibadani, kwa Mola wetu Jalia
Tuoneeni imani, vijana twawalilia
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?
5. Na la kuzingatia, hamukosi kwa Rabana
Kwenye kutusaidia, tunapo kwaruzana
Tapungua na udhia, hilo fahamu sana
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?
6. Beti sita nimetimu, naweka kalamu chini
Rabi ndiwe ni hakimu, uhukumuo Manani
Vijana tunalaumu, wakutusikiza ni nani?
Kuna ubaya gani, kuwaangalia walooana?